DP Ruto Aweka Wazi Susan Kihika Ndiye Kipenzi Chake Nakuru

Publish date: 2024-09-08

Naibu Rais William Ruto Jumamosi Oktoba 2 alionyesha wazi kuwa Seneta wa Nakuru Susan KIhika ndiye kipenzi chake katika siasa za kaunti hiyo.

Ruto alikubali mwaliko wa Kihika kuhudhuria kikao na hustlers wa Nakuru katika nyumbani kwa seneta huyo.

Mwaliko huo ulikuwa pia nafasi ya Kihika kukaribisha Ruto na wafuasi wa UDA katika makao yake mapya huko Ngata.

Wafuasi hao walipata nafasi ya kuingia katika boma hilo ambalo limeundwa hivi maajuzi likitajwa kama mojawapo wa mikakati ya Kihika kuwania ugavana Nakuru.

Wakosoaji wa Kihika wamekuwa wakimlima kwa kukosa kuwa na boma kaunti ya Nakuru na kuhoji ni vipi ataongoza wakazi kutoka Nairobi.

Pia soma

Kahawa ya kutoka Afrika Yazidi Kupata Umaarufu nchini China

Sasa amewajibu kwa kuunda boma la kifahari ambalo pia limezua gumzo wa ni vipi amekuwa akiuza sera za hustlers na yeye ni wazi ana mifuko mizito.

Baada ya kikao nyumbani kwa Kihika, Ruto alizuru Nakuru mjini huku akiandamana na Kihika sako kwa bako.

Kama ishara ya kuwa Kihika ndiye chaguo lake, DP alikuwa kwenye gari moja naye wakati wa kuhutubia wakazi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZ4VzhJRmm6lloqrBsHnAsJykmV2srru1jKysrJmeYriqtMikmGamlJ7GpnnKoqeepqqeeqS0wKScZqaRoMKzwY2hq6ak